Matangazo ya moja kwa moja ya TV
HABARI
MATUKIO YA KISIASA
MATUKIO YA AFRIKA
MASUALA YA JAMII
MICHEZO
HABARI KWA LUGHA YA KIINGEREZA
Unaweza kusikiliza matangazo yetu hapa

Kusikiliza matangazo, tafadhali bonyeza alama ya spika ya masikioni hapo chini, na kuwasiliana nasi: kiswahili@dw.com

Kusikiliza matangazo ya Idhaa ya Kiswahili ya DW, tafadhali bonyeza alama ya spika ya masikioni hapo chini, na kuwasiliana nasi, tafadhali tuandikie moja kwa moja kupitia: kiswahili@dw.com

Vidio

04:25 dakika.
Media Center | 23.12.2022

Jasiri katika kilimo biashara

02:23 dakika.
IDHAA YA KISWAHILI | 22.12.2022

Ujerumani yarejesha vinyago vya Nigeria

02:30 dakika.
IDHAA YA KISWAHILI | 22.12.2022

Utamaduni wa Wachaga kuwaenzi mababu

02:52 dakika.
IDHAA YA KISWAHILI | 21.12.2022

Wanajeshi wa kike Ukraine wapata magwanda

Vidio, Sauti na Picha Zote
TUFUATILIE KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII
2022: Mwaka wa kufikwa na mabadiliko ya tabia nchi
Ulaya: Joto na ukame kuliko siku za nyuma

Majira ya joto ya Ulaya yalishuhudia joto kali na ukame mbaya zaidi katika miaka 500. Zaidi ya watu 500 walikufa kutokana na joto nchini Uhispania huku kiwango cha joto kikifikia nyuzi joto 45. Nchini Uingereza, joto lilipindukia nyuzi 40. Maeneo mengine ya mabara kulikuwa na ukame zaidi, maeneo mengi yalikuwa na shida ya maji.

2022: Mwaka wa kufikwa na mabadiliko ya tabia nchi
Moto wa msituni ulizagaa Ulaya yote

Kuanzia Ureno, Uhispania na Ufaransa hadi Italia, Ugiriki, Cyprus na Siberia kwa upande wa Kaskazini, bara hilo liliwaka moto. Moto umeteketeza hekta 660,000 ikiwa sawa na eka 1,630,896) za ardhi hadi katikati ya mwaka - ni kubwa zaidi tangu kuanza kuwekwa rekodi 2006.

2022: Mwaka wa kufikwa na mabadiliko ya tabia nchi
Janga la mafuriko Asia

Mvua kubwa za masika ziliikumba Pakistan,na kuzamisha theluthi ya taifa eneo la nchi. Mafuriko hayo yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 1100, kuacha wengine milioni 33 bila makazi na kusababisha kuenea kwa magonjwa. Hali kama hiyo iliikumba Afghanistan. Mafuriko hayo yaliharibu maelfu ya hekta za ardhi, na hivyo kuzidisha njaa kali nchini humo.

2022: Mwaka wa kufikwa na mabadiliko ya tabia nchi
Joto kali na vimbunga vinakumba bara hilo pia

Kabla ya mafuriko, Afghanistan, Pakistan na India zilikumbwa na joto kali na ukame. China, wakati huo huo ilikumbana na ukame wake mbaya zaidi katika miaka 60 na joto kali. Kufikia msimu wa vuli vimbunga 12 tayari vilikuwa vimepiga nchini humo. Dhoruba kubwa pia ilipiga Ufilipino, Japan, Korea Kusini na Bangladesh. Mabadiliko ya hali ya tabia nchi yanafanya dhoruba kama hizo kuwa na nguvu zaidi.

2022: Mwaka wa kufikwa na mabadiliko ya tabia nchi
Madhara ya makubwa ya mabadiliko ya tabia nchi Afrika

Afrika ipo katika joto kali na kwa kasi zaidi kuliko kuliko mabara mengine. Hali hiyo inasababisha maafa makubwa kutokana na mabadiliko ya unyeshaji wa mvua, ukame na mafuriko. Somalia inakabiliana na ukame mbaya zaidi katika kipindi cha miaka 40. Mgogoro huo umewalazimu zaidi ya watu milioni moja kuyahama makazi.

2022: Mwaka wa kufikwa na mabadiliko ya tabia nchi
Uhamiaji na njaa katika bara la Afrika

Mafuriko na ukame mkubwa umefanya kilimo na ufugaji kutowezekana katika sehemu fulani za Afrika. Kwa hivyo, mamilioni ya watu wanakabiliwa na Wengi hadi sasa tayari wamepoteza maisha kwa njaa hiyo nchini Ethiopia, Somalia na Kenya.

2022: Mwaka wa kufikwa na mabadiliko ya tabia nchi
Moto na mafuriko huko Amerika Kaskazini

Dhoruba kali zilikumba majimbo ya Marekani ya California, Nevada na Arizona. Janga la moto liliyaunguza majimbo yote matatu katika halijoto ya zaidi ya nyuzi 40 C mwishoni mwa msimu wa kiangazi. Kinyume chake, mvua kubwa iliyonyesha mapema wakati wa kiangazi ilisababisha mafuriko makubwa katika Mbuga ya Kitaifa ya Yellowstone, pamoja na Kentucky.

2022: Mwaka wa kufikwa na mabadiliko ya tabia nchi
Vimbunga vimeivuruga Marekani

Mwezi Septemba, Kimbunga Ian kililiharibu jimbo la Florida. Mamlaka za eneo hilo zilielezea uharibifu huo kama "wa kihistoria" kwa ukubwa. Hapo awali Ian kilishambulia Cuba, ambapo wakazi walikosa umeme kwa siku kadhaa. Fiona kimekuwa kimbunga kibaya zaidi cha kitropiki kuwahi kuipiga Canada baada ya awali kuyaathiri maeneo ya Amerika ya Kusini na Carribean.

2022: Mwaka wa kufikwa na mabadiliko ya tabia nchi
Dhoruba mbaya za kitropiki huko Amerika ya Kati

Fiona haikuwa dhoruba pekee iliyopiga Amerika ya Kati. Mnamo Oktoba, Kimbunga Julia kilipiga Colombia, Venezuela, Nicaragua, Honduras na El Salvador, na kusababisha uharibifu mkubwa. Kuongeza joto duniani kunaongeza halijoto baharini, jambo ambalo linasababisha hali mbaya ya vimbunga.

2022: Mwaka wa kufikwa na mabadiliko ya tabia nchi
Ukame mkubwa Amerika ya Kusini

Ukame unaoendelea kukumba karibu bara zima la Amerika Kusini. Chile, kwa mfano, imekuwa ikikabiliwa na ukosefu wa mvua uliokithiri tangu 2007. Katika mikoa mingi, vijito na mito imepungua kwa kati ya 50 na 90%. Mexico haijapata mvua kwa miaka kadhaa mfululizo. Argentina, Brazil, Uruguay, Bolivia, Panama na sehemu za Ecuador na Colombia pia wanaishi na ukame.

2022: Mwaka wa kufikwa na mabadiliko ya tabia nchi
Mafuriko New Zealand na Australia

Mvua kubwa ilisababisha mafuriko makubwa Australia mara kadhaa 2022. Kati ya Januari na Machi, pwani ya mashariki ya nchi ilifikwa na takriban kiwango cha sawa na inachopata Ujerumani kwa mwaka mmoja. New Zealand haikuepuka mafuriko.

| 11
Jinsia na Mwili