1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

47 WAUWAWA MOSUL

11 Machi 2005

MOSUL:

Si chini ya watu 47 wameuwawa katika hujuma ya mtu aliejitoa mhanga katika mji wa Mosul, kaskazini mwa Iraq.Hii ni kwa muujibu wa taarifa za wakuu katika hospitali 2 kuu ambako watu hao walipelekwa.Kiasi cha watu wengine 100 wamejeruhiwa .Hujuma hii imetokea wakati waombolezi walipokusanyika katika ukumbi mmoja karibu na msikiti kwa mazishi ya waumini wa madhehebu ya shiia.