1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

ABUJA: majeshi ya Nigeria yaua wapiganaji wa kiislamu 25

19 Aprili 2007

Majeshi ya Nigeria yamesema yamewaua wapiganaji wa kiislamu 25 katika mji wa Kano kaskazini mwa nchi hiyo.

Katika shambulio moja kubwa majeshi hayo yaliwazingira wapiganaji hao ambao hapo awali walikiteka kituo cha polisi na kuwaua polisi 13.

Wakati huo huo vyama vya upinzani vya Nigeria vinataka uchaguzi wa rais wa jumamosi ijayo uahirishwe kufuatia madai juu ya hitilafu zilizotokea katika uchaguzi wa majimbo mwishoni mwa wiki iliyopita.

Usalama umeimarishwa nchini kote baada ya vifo vya watu 20 wakati wa uchaguzi huo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW