1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

ABUJA:40 wameshakufa kutokana na ghasia zinazoandamana na uchaguzi nchini Nigeria

16 Aprili 2007

Watu zaidi ya 40 wamekufa kutokana na ghasia zilizoandamana na uchaguzi wa wabunge na magavana nchini Nigeria.

Matokeo ya awali yameonesha kuwa chama kinachotawala cha PDP kinaongoza katika majimbo sita kati ya manane ambapo kura zimehesabiwa .

Habari juu ya matokeo hayo zimesababisha ghasia katika mitaa kadhaa.Wapinzani wa serikali walichoma moto majengo na kuweka vizuizi barabarani.

Hatahivyo rais Olusegun Obasanjo amesema anatumai kuwa matokeo ya uchaguzi huo yatakuwa halali.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW