1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Afghanistan yaapa kulipiza kisasi dhidi ya Pakistan

18 Machi 2026

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Afghanistan Sirajuddin Haqqani amesema watalipiza kisasi kwa shambulio la anga la Pakistan lililoua mamia ya watu katika kituo cha kurekebisha tabia kwa waraibu wa dawa za kulevya cha Kabul.

Afghanistan Kabul 2026 | shambulizi
Uharibu uliofanywa na Pakistan katika kituo cha matibabu ya waraibu wa dawa za kuelevya mjini KabulPicha: Wakil Kohsar/AFP

Wakati wa mazishi ya baadhi ya waliouawa mjini Kabul, Haqqani amesema watalipiza kisasi na akawataja waliohusika katika shambulizi hilo la Jumatatu usiku kuwa ''wahalifu.''

Mamlaka ya Taliban imesema takriban watu 400 waliuawa na zaidi ya 200 kujeruhiwa katika shambulizi hilo ambalo ndilo baya zaidi kutokea katika mgogoro wa sasa kati ya mataifa hayo mawili jirani.

Hata hivyo Pakistan imekanusha madai ya  serikali ya Taliban kwamba kituo hicho kililengwa kwa makusudi na kusema kililenga kushambulia kambi za kijeshi na miundombinu ya msaada kwa magaidi.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW