1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Afghanistan yadai Pakistan imeishambulia na kuuwa raia wake

22 Februari 2026

Pakistan imesema imeshambulia maeneo ya wanamgambo nchini Afghanistan baada ya kudai kuwa wanamgambo hao wamekuwa wakitekeleza mashambulizi nchini mwake hasa katika mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Afghanistan Bihsud 2026 | Taliban-Sicherheitskräfte suchen Opfer nach pakistanischem Luftangriff
Afghanistan yasema wanawake na watoto ni miongoni mwa waliouawa katika shambulizi la Pakistan nchini mwake Picha: AFP

Pakistan imesema wanamgambo hao wanaishambulia nchi hiyo kutoka Kabul.

Utawala wa Taliban umesema wanawake na watoto ni miongoni mwa watu 18 waliouwawa na wengine wengi waliojeruhiwa katika shambulizi la Jana Jumamosi. Wizara ya ulinzi ya Afghanistan imesema inapanga shambulio la kulipiza kisasi, hali ambayo inahofiwa kuzidi kutia doa mahusiano ya mataifa hayo mawili.

Shambulizi hili limetokea siku kadhaa baada ya Afghanistan kuwaachia huru wanajeshi watatu wa Pakistan katika juhudi zilizosimamiwa  na Saudi Arabia kwa nia ya kupoza mvutano kati ya pande hizo mbili kufuatia miezi kadhaa ya makabiliano makali ya mpakani.

Pakistan inaituhumu Afghanistan kutoa hifadhi kwa makundi ya wapiganaji wanaotishia usalama wa mipaka yake madai ambayo watawala wa Taliban wamekuwa wakiyakanusha.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW