1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Timu nyengine 3 za Afrika zafuzu kushiriki Kombe la Dunia

15 Oktoba 2025

Afrika Kusini, Ivory Coast na Senegal zimefuzu kushiriki kombe la dunia la kandanda mwaka 2026 kwa kushinda mechi zao Jumanne na kujaza nafasi tatu zilizokuwa zimesalia kati ya tisa zilizotengewa bara la Afrika.

Kinshasa | Mechi ya kufuzu kushiriki Kombe la dunia kati ya DRC na Senegal
Mchezaji wa Senegal, Nicolas Jackson akishangilia baada ya kufunga bao katika mechi ya Kundi B ya kufuzu Kombe la Dunia 2026 kati ya DR Congo na Senegal kwenye Uwanja wa Martyrs' mjini Kinshasa, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Jumanne, Septemba 9, 2025.Picha: Samy Ntumba Shambuyi/AP Photo/picture alliance

Timu hizi tatu zinajiunga na Algeria, Cape Verde, Misri, Morocco, Senegal na Tunisia katika mashindano hayo yatakayoandaliwa nchini Marekani, Canada na Mexico.

Timu za Cameroon, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Gabon na Nigeria zimeyaweka hai matumaini yao ya kujaza nafasi ya kumi kwa bara la Afrika na zitacheza mechi moja moja za nusu fainali na fainali itakayochezwa nchini Morocco mwezi ujao wa Novemba na washindi watafuzu kwa michuano hiyo yakombe la dunia mwaka 2026.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW