1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Afrika mashariki itapoteza sifa kuwa chimbuko la binadamu?

Caro Robi
30 Novemba 2018

Wataalamu wa utafiti wa mambo ya kale nchini Algeria, wamegundua zana zilizotengenezwa kwa mawe na mifupa ya wanyama iliokatwa ambayo huenda vina umri wa hadi miaka milioni 2 na laki 4.

Lake Turkana National Parks
Picha: AFP/Getty Images/Y. Chiba

Wataalamu wa utafiti wa mambo ya kale nchini Algeria, wamegundua zana zilizotengenezwa kwa mawe na mifupa ya wanyama iliokatwa ambayo huenda vina umri wa hadi miaka milioni 2 na laki 4, na hivyo kusababisha utata juu ya eneo la Afrika mashariki kuwa chimbuko la binadamu.

Kwa mujibu wa utafiti uliochapishwa Alhamisi na jarida la Sayansi ugunduzi huo umetokea katika Setif kilomita zipatazo 300 mashariki mwa mji mkuu Algiers, kutokana na utafiti wa kikudi cha wataalamu wa kimataifa wakiwemo kutoka Algeria.

Vifaa hivyo vinafanana na vile vinavyoitwa Oldwan, vilivyogunduliwa Afrika Mashariki.

Wataalamu wanaashiria  kwamba  watangulizi wa binadamu wa leo waliishi Afrika kaskazini kwa karibu miaka 600,000 kabla kuliko ilivyokuwa ikidhaniwa na wanasayansi.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW