Afya ya Besigye yadaiwa kudhoofika
20 Januari 2026
Matangazo
Katika taarifa yake, chama hicho kimesema kuwa Besigye yuko katika hali mbaya kiafya. Aidha, kimetoa wito kwa maafisa wa Uganda kuhakikisha madaktari binafsi pamoja na familia yake wanaonana naye bila vikwazo vyovyote.
Chama hicho kimeendelea kusema ni jambo la kusikitisha kwamba mtu ambaye amejitolea maisha yake kwa afya na uhuru wa wengine ananyimwa haki yake ya kupata utu wa matibabu.
Kwa upande wake, msemaji wa mfumo wa magereza nchini humo Frank Baine, amekanusha taarifa hiyo ya afya ya Besigye na kusema kupelekwa kwake hospitalini kulikuwa kwa ajili ya uchunguzi wa jumla na kwamba leo asubuhi alikuwa akifanya mazoezi yake.