1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaVatican

Afya ya Papa wa zamani bado ni tete

29 Desemba 2022

Aliyekuwa kiongozi wa kanisa katoliki Papa Benedict wa 16 bado yuko katika hali mbaya lakini chini ya uangalizi wa madaktari.

Vatikan Papst Benedikt XVI. leitet die Palmsonntagsmesse im Vatikan
Picha: Vandeville Eric/ABACA/picture alliance

Tamko hili linatolewa siku moja baada ya makao makuu ya Vatican kufichua kuwa afya ya papa huyo mstaafu Mjerumani mwenye umri wa miaka 95 imedhoofika. Taarifa kutoka kwa msemaji wa Vatican Matteo Bruni imesema Benedict ana fahamu na yuko imara, lakini hali yake haijabadilika tangu jana. Benedict, ambaye katika mwaka wa 2013 alikuwa papa wa kwanza tangu Zama za Kati kujiuzulu kama kiongozi wa kanisa katoliki ulimwenguni, amekuwa katika hali ya afya iliyodhoofika kwa miaka mingi na hutumia kiti cha walemavu. Kiongozi wa sasa Papa Francis alisema jana kuwa mtangulizi wake huyo ambaye jina lake la kuzaliwa ni Joseph Ratzinger, ni mgonjwa sana na akawahimiza watu kumuombea.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW