Akili ya kubuni (AI) imeendelea kukuwa na hata kutumika katika sekta mbalimbali ikiwemo rasmi na zile ambazo si rasmi. Kundi la wanafunzi nalo halijabaki nyuma, wanatumia teknolojia hii pia. Lakini lipo kundi ambalo lina wasiwasi kwamba matumizi yaliokithiri ya akili ya kubuni yanaweza kuhatarisha maendeleo ya akili ya binadamu katika kufikiri.