1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Alonso amfagilia Jude Bellingham

26 Juni 2025

Kocha mpya wa Real Madrid Xabi Alonso amesema "anafurahishwa" na mchezo wa kiungo wa kati wa timu hiyo Jude Bellingham.

Jude Bellingham
Jude Bellingham anachukuliwa kama mmoja ya wachezaji bora kabisa kwenye kikosi cha Real Madrid ya UhispaniaPicha: Lluis Gene/AFP/Getty Images

Siku ya Jumapili, Bellingham alifunga goli lake la kwanza akiwa chini ya Alonso, wakati Real Madrid ilipoilaza klabu ya Pachuca ya Mexico, kwenye michuano ya Kombe la Dunia la Vilabu.

Manguli hao "Los Blancos" watamalizia mbio za makundi kwa kukipiga na RB Salzburg huko Philadelphia, na ikiwa watashinda watasonga mbele kwenye raundi ya 16 bora wakiwa vinara wa Kundi H.

Timu zote mbili zina pointi sawa baada ya michezo miwili, huku timu ya Al Hilal ya Saudi Arabia ikiwa na pointi 2.

Jude Bellingham akiichezea timu yake ya taifa ya England kwenye michauno y UEFA Euro 2024Picha: INA FASSBENDER/AFP/Getty Images

"Ni wazi, ataendelea kuwa mchezaji muhimu kwetu," alisema Alonso alipomzungumzia Bellingham kwenye mkutano na waandishi wa habari kabla ya mechi. "Ninapenda anachofanya anapokuwa uwanjani na jinsi anavyojituma kwenye michezo yote.

"Ana ubora wa hali ya juu, tuliona alivyocheza dhidi ya Pachuca, na tupo karibu naye wakati wote. "Jude ana matamanio mengi, anataka kuimarika na kuendelea kukua, na tunataka kuendelea kuona jinsi anavyokua."

Kylian Mbappe ameachwa kwenye kikosi cha Real Madrid, licha ya kurejea kwenye mazoezi siku ya Jumatano baada ya kuugua.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW