Haki za binadamuUganda
Amnesty: Uganda inawakandamiza wapinzani kabla ya uchaguzi
5 Januari 2026
Matangazo
Uganda inatarajiwa kufanya uchaguzi Januari 15.
Shirika hilo limekusanya vithibitisho vya maafisa wa usalama kuwapiga na kutumia gesi ya kutoa machozi dhidi ya wafuasi wa chama cha upinzani cha National Unity Platform NUP kinachoongozwa na Bobi Wine.
Mkurugenzi wa Amnesty wa kanda ya mashariki na kusini mwa Afrika Tigere Chagutah amesema, serikali imeanzisha kampeni ya kikatili ya kuwakandamiza wapinzani na wafuasi wao hali inayowawekea mazingira magumu ya kufanya mikusanyiko ya amani.
Aidha, upo wasiwasi kwamba huenda serikali ikazima intaneti wakati wa uchaguzi, kama ilivyofanya mwaka 2021 ili kuzuia usambazaji wa taarifa kuhusiana na udanganyifu wa kura na machafuko.