1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Amnesty yakosoa hatua za Trump akitimiza siku 100 madarakani

29 Aprili 2025

Shirika la kimataifa la kutetea haki za binaadamu la Amnesty International limetoa Jumanne ripoti yake ya kila mwaka na kukosoa vikali hatua za rais wa Marekani Donald Trump, ambaye ametimiza siku 100 akiwa madarakani.

Nembo ya Shirika la Kimataifa la kutetea haki za binaadamu la Amnesty International
Nembo ya Shirika la Kimataifa la kutetea haki za binaadamu la Amnesty InternationalPicha: Britta Pedersen/dpa/picture alliance

Amnesty imesema hatua za Trump zinalenga kurejesha nyuma mafanikio yaliyopatikana katika vita dhidi ya umaskini duniani, kupambana na ubaguzi wa rangi na vipaumbele muhimu vya haki za binadamu.

Tangu alipoapishwa kuongoza muhula wa pili mnamo Januari 20, Trump amechukua hatua kadhaa ambazo zimeutikisa ulimwengu  kiuchumi, kijamii na kiusalama.

Baadhi, ni hatua za ushuru, kusitisha misaada ya kimataifa, sintofahamu na washirika wake wa NATO pamoja na vitisho vya kunyakuwa maeneo kama Gaza, Greenland, Mfereji wa Panama na kutaka kuifanya Canada kuwa jimbo la 51 la Marekani.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW