Amnesty yaonya Kombe la Dunia kuwa 'jukwaa la ukandamizaji'
30 Machi 2026
Matangazo
Ripoti ya shirika hilo yenye kurasa 36 iliyopewa jina "Ubinaadamu Lazima Ushinde: Kulinda haki, kukabiliana na ukandamizaji kwenye Kombe la Dunia la FIFA 2026" inachambuwa kwa kina matukio yanayoweza kuhatarisha haki za mashabiki, wachezaji, waandishi wa habari, wafanyakazi na jamii za wenyeji kwenye mataifa hayo matatu.
Ikiwa ni miezi michache kuelekea michuano hiyo, Marekani bado imeweka marufuku ya kuingia nchini humo kwa baadhi ya nchi ambazo zimefaulu kushiriki kombe hilo litakalokuwa na mechi 48.
Michuano hiyo inayotazamiwa kuhudhuriwa na mamilioni ya mashabiki wa soka inaanza mnamo Juni Mosi kwa maechi kati ya Meksiko na Afrika Kusini.