1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Amri ya kutotoka nje yawekwa BurkinaFaso kupambana na ugaidi

5 Machi 2023

Burkina Faso imeweka maeneo ya Kaskazini na sehemu ya katikati ya Mashariki mwa nchi chini ya amri ya kutotoka nje ili kuzisaidia juhudi za kupambana na makundi ya wapiganaji wenye itikadi kali.

Operation Barkhane in Mali
Picha: Philippe De Poulpiquet/MAXPPP/dpa/picture alliance

Uasi wa muda mrefu katika taifa hilo la Sahel umesbabisha mauaji ya maelfu ya watu, polisi na wanajeshi huku zaidi ya watu milioni mbili wakikimbia  makaazi yao. 

Taarifa ya Katibu Mkuu ya serikali ya jimbo la Kaskazini, Kouilga Albert Zongo imesema chini ya mpango wa kupambana na ugaidi amro ya kutotoka nje usiku itaanza kutekelezwa kuanzia saa nne usiku hadi saa kumi na moja alfajiri kuanzia tarehe 3 hadi tarehe 31 mwezi Machi. 

Amri hiyo pia imepiga marufuku magari na pikipiki kuwepo barabarani ndani ya muda huo uliotolewa. Zongo amesema amri hiyo itaisadia jeshi kupambana na ugaidi katika eneo hilo linalopakana na Mali kulikoanzia uasi mwaka 2015.
 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW