1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

AMSTERDAM: Vyama vyashauriana kwa faragha kuhusu kuunda serikali ya muungano.

3 Januari 2007

Mashauriano yanaendelea nchini Uholanzi ili kuunda serikali ya muungano.

Chama cha mrengo wa kushoto cha Waziri Mkuu wa muda Jan Peter Balkenende kinaendesha mashauriano ya faragha na chama cha Labour na chama kingine kidogo cha kidini.

Jaribio la kwanza la kuunda serikali ya mseto liligonga mwamba mwezi Novemba baada ya vyama husika kukosa kukubaliana kuhusu sera.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW