1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

ANC yaonekana kushindwa kupata wingi wa viti bungeni

1 Juni 2024

Zoezi la kuhesabu kura linaingia siku yake ya mwisho baada ya uchaguzi wa bunge kumalizika nchini Afrika kusini. Chama tawala cha African National Congress (ANC) kinaonekana kushindwa kupata wingi wa viti bungeni.

Uchaguzi wa Afrika Kusini 2024
ANC yaonekana kushindwa kupata wingi wa viti bungeni Picha: Jerome Delay/AP Photo/picture alliance

ANC imekuwa ikishinda katika kila chaguzi ya kitaifa nchini humo tangu uchaguzi wa kihistoria uliofanyika mwaka 1994 uliomaliza utawala wa wazungu.

Lakini ndani ya muongo mmoja uliopita umaarufu wake ulianza kushuka baada ya waafrika kusini kushuhudia uchumi kuyumba na kutokuwa inavyohitajika, kupanda kwa viwango vya ukosefu wa ajira, na uchakavu wa miundo mbinu. 

Huenda Afrika Kusini ikaunda serikali ya mseto

Matokeo yanayoendelea kutolewa baada ya kura kuhesabisha katika zaidi ya asilimia 97 kati ya vituo 23,000 vya kupigia kura katika uchaguzi huo uliofanyika siku ya Jumatano, ANC imepata asilimia 40.11 ya kura ikiwa imeshuka kutoka asilimia 57.50 iliyopata katika uchaguzi uliopita wa mwaka 2019. 

Chama kikuu cha upinzani cha the Democratic Alliance, kimepata asilimia 21.72 ya kura zilizohesabiwa hadi sasa huku chama cha uMkhonto we Sizwe (MK), chama kipya kinachoongozwa na rais wa zamani Jacob Zuma kikipata asilimia 14.83 ya kura.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW