1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

ANKARA: Erdogan aonywa asigombee urais

14 Aprili 2007

Zaidi ya waandamanaji elfu 20 wamefanya maandamano kumuonya waziri mkuu wa nchi hiyo Recep Tayyip Erdogan dhidi ya kugombea kiti cha urais katika uchaguzi wa mwezi ujao nchini Uturuki.

Waandamanaji hao walipeperusha vibendera vyekundu na kuimba nyimbo za kuupinga uislamu.

Waandamanaji hao wanahofia kuwa iwapo Erdogan atashinda katika uchaguzi huo basi huenda akapitisha sharia za kiislamu nchini humo.

Ingawa Uturuki haitawaliwi kwa misingi ya dini ya kiislamu lakini dini kuu nchini humo ni ya kiislamu.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW