1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Annan ataka kipelekwe kikosi cha amani Burundi

20 Machi 2004
NEW YORK: Katibu Mkuu wa UM Kofi Annan ameliita Baraza la Usalama lipeleke kikosi cha kuhifadhi amani nchnini Burundi. Nchi hiyo ya Afrika ya Kati ina nafasi nzuri wakati huu kurejeshewa hali yake ya usalama miaka kmumi baada ya kumalizika vita vya ndani. Kwa ajili hiyo hadi hapo tarehe 2 April UM utapaswa kupokea dhamana ya hifadhi ya amani kutoka nchi za UA. Bwana Annan ameshauri kipelekwe kikosi cha wanajeshi 5,650 cha UM. Baraza la Usalama la UM litaijadili hali ya Burundi hapo Jumatatu.
Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW