1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Armenia na Azerbaijan zalumbana upya

Josephat Charo
20 Juni 2024

Armenia za Azerbaijan zimepigana vita mara mbili tangu kusambaratika kwa Muungano wa zamani wa Urusi mwanzoni mwa miaka ya 1990, huku Azerbaijan ikiyachukua maeneo makubwa ya ardhi 2020.

Hikmet Hajiyev. mshauri wa sera za kigeni wa rais wa Azerbaijan, Ilham Aliyev
Hikmet Hajiyev. mshauri wa sera za kigeni wa rais wa Azerbaijan, Ilham AliyevPicha: DW

Armenia na Azerbaijan zimelumbana upya kwa maneno makali jana Jumatano baada ya Ufaransa kuahidi kuipelekea silaha mpya Armenia.

Nchi hizo mbili katika eneo la Caucasus Kusini zimepania kupiga hatua miezi ya hivi karibuni katika utekelezaji wa mkataba wa amani unaojumuisha uwekaji wa mipaka, huku Armenia ikikubali kukabidhi vijiji vinne vya mpakani vinavyozozaniwa kwa Azerbaijan.

Tangazo la Jumanne wiki hii la waziri wa ulinzi wa Ufaransa Sebastien Lecornu kwamba Ufaransa ingeiuzia silaha Armenia limezua ukosoaji mkali kutoka kwa Azerbaijan. 

Soma pia: Kiongozi wa Armenia asema mkataba wa amani na Azerbaijan wakaribia

Hikmet Hajiyev, mshauri wa cheo cha juu wa sera ya kigeni kwa rais wa Azerbaijan Ilham Aliyev ameviambia vyombo vya habari vya Azerbaijan kwamba hawaichukulii sera ya Ufaransa katika eneo la Caucasus Kusini kuwa na tija na ni sera mbaya yenye madhara.

Hajiyev amesema sera hiyo ni pigo kwa mahusiano kati ya Azerbaijan na Armenia.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW