1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAzerbaijan

Armenia yataka kuwepo ujumbe wa UN huko Nagorno Karabakh

24 Septemba 2023

Waziri wa Mambo ya Nje wa Armenia, Ararat Mirzoyan imeishutumu Jumuiya ya kimataifa kwa kutochukua hatua kufuatia operesheni ya kijeshi ya Azerbaijan ya kuchukua udhibiti wa mkoa unaozozaniwa wa Nagorno-Karabakh.

Konflikt in Berg-Karabach
Picha: Emmanuel Dunand/AFP

Akizungumza kwenye Mjadala Mkuu wa Umoja wa Mataifa mjini New York jana Jumamosi, Mirzoyan amesema jumuiya ya kimataifa na Umoja wa Mataifa zimeshindwa kuwaokoa watu.

Waziri huyo ametoa wito wa kuwepo kwa ujumbe wa Umoja wa Mataifa utakaofuatilia hali jumla ya haki za binadamu pamoja na usalama katika eneo hilo.

Nagorno-Karabakh  ni sehemu ya Azerbaijan lakini sehemu kubwa ya wakaazi wake ni jamii ya Waarmenia. Kwa muda mrefu udhibiti wa eneo hilo umekuwa chanzo cha mzozo kati ya mataifa hayo mawili yaliyokuwa hapo zamani katika Muungano wa Kisovieti.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW