1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Askari wa zamani aliyehukumiwa kwa mauaji ya Rwanda afariki

11 Juni 2023

Mwanajeshi wa zamani aliyehukumiwa kwa kuchochea mauaji ya kimbari nchini Rwanda mwaka wa 1994 amefariki nchini Niger baada ya ombi lake la kupewa msaada wa matibabu nchini Uingereza kutojibiwa.

Gedenken an den Genozid in Ruanda
Picha: Ben Curtis/AP/picture alliance

Tharcisse Muvunyi alikuwa katika jeshi la Rwanda wakati Wahutu walio wengi wenye misimamo mikali waliwauwa zaidi ya watu 800,000 kutoka kabila la walio wachache la Tutsi na Wahutu wa misimamo ya wastani katika siku 100.  Wakili wake Abbe Jolles amesema Muvunyi alipatikana jana mchana akiwa amefariki bafuni.

Muvunyi luteni kanali wa zamani aliishi katika nyumba salama katika eneo lisilojulikana nchini Tanzania baada ya kuachiwa huru 2012 na akahamia Niger 2021 katika nyumba ya watu saba wengine waliokuwa wameshitakiwa kwa mauaji hayo ya halaiki.

Alikamatwa nchini Uingereza, akahukumiw akifungo cha miaka 15 jela mwaka wa 2010 na akaachiliwa huru miaka miwili baadae baada ya muda aliotumikia.

Alikuwa mgonjwa kwa wiki kadhaa, na wakili wake Jolles akaufahamisha Umoja wa Mataifa kuwa Muvunyi alihitaji matibabu ya dharura Uingereza. Lakini hakupata jibu.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW