1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Athari za tumbaku ni tele kwenye mazingira: ripoti ya WHO

31 Mei 2022

Ripoti mpya ya shirika la Afya Duniani, WHO, kuhusu madhara ya tumbaku, imetahadharisha kwamba mbali na uvutaji sigara kusababisha madhara makubwa kiafya, pia huathiri mazingira.

qualmende Zigarette in einer Hand
Picha: Imago Images/Sven Simon/F. Hoermann

Kulingana na takwimu kwenye ripoti hiyo ya shirika la Afya Duniani, WHO, kuhusu madhara ya tumbaku, kila mwaka uzalishaji na matumizi ya tumbaku husababisha vifo vya watu milioni nane ulimwenguni kote.

Huchangia kukatwa kwa miti milioni 600 kila mwaka, hekari 200,000 za ardhi kutumika, pamoja na tani bilioni 22 ya maji. Isitoshe huzalisha takriban tani milioni 84 ya hewa ukaa angani, hali inayochafua pakubwa sayari yetu dunia.

Ripoti hiyo ambayo imechapishwa Jumanne, siku ya kuhamasisha kuhusu madhara ya tumbaku kote ulimwenguni, imetahadharisha kuwa hewa chafu kutokana na uzalishaji wa tumbaku na usafirishaji wake, ni sawa na moja juu ya tano ya hewa ukaa ambayo hutolewa na sekta ya ndege za usafirishaji kila mwaka, dhihirisho kwamba sekta hiyo inachangia ongezeko la joto ulimwenguni.

Bidhaa za tumbaku zina zaidi ya kemikali hatari 7,000 ambazo huishia katika mazingira yetu kila zinapotupwa, amesema Rüdiger Krech, mkurugenzi wa idara ya uhamasishaji wa masuala ya afya katika WHO.Picha: picture-alliance/AP Photo/Ahn Young-joon

Uchafuzi wa vichujio vya sigara katika mazingira

Kila mwaka, takriban vipande trilioni 4.5 vya sigara huishia kwenye mito na bahari, sakafuni, ardhini na kwenye fukwe. Shughuli za kuokota taka za sigara katika mazingira yetu ni mzigo ambao raia wa kawaida walipao ushuru, hulazimika kugharamia, badala ya sekta hiyo yenyewe.

Ripoti ya WHO imetoa wito kwa mataifa kuiwajibisha sekta ya tumbaku kuhakikisha inabeba jukumu la kusafisha taka za bidhaa hiyo.

Imependekeza pia vipande vya sigara vinavyotumika kama vichujio vipigwe marufuku, ikisema vina vipande vidogovidogo vya plastiki na huchangia pakubwa katika uchafuzi wa mazingira. Licha ya hatari hizo, faida za tumbaku kiafya bado hazijathibitishwa.

Athari ya tumbaku kwa wakulima

Wakulima wa kila siku wa tumbaku huwa katika hatari kubwa ya kuathiriwa na nikotini kutokana na tumbaku, sawa na wavutao sigara 50 kila siku.Picha: Michael Runkel/imagebroker/imago images

Kwa upande mwingine, wakulima wa tumbaku huathiriwa na magonjwa yanayotokana na hewa ukaa au athri za kemikali aina ya nikotini ambayo huingia mwilini kupitia ngizi zao.

Kampuni ya tumbaku yatuhumiwa kuwahujumu washindani wake Afrika

Kulingana na Krech, inakadiriwa kwamba wakulima wanaoshughulika na tumbaku kila siku, nikotini inayotokana na sigara 50 huingia mwilini mwao kila siku. Amesema hali hii inatia wasiwasi sana hususan kwa Watoto wanaohusishwa kwenye kilimo cha tumbaku.

"Hebu fikiria, mtoto mwenye umri wa miaka 12 anakua katika mazingira ambapo yuko sawa na anayevuta sigara 50 kila siku,” amesema Krech.

Saratani ya kinywa

02:56

This browser does not support the video element.

Nchi masikini huongoza kuzalisha tumbaku; WHO

Mara nyingi, kilimo cha tumbaku hufanywa katika mataifa masikini. Katika nchi hizo, mashamba ya tumbaku hayapati maji ya kutosha.Ripoti imeeleza kuwa kinachosikitisha ni kwamba wakulima huendeleza kilimo hicho badala ya mazao muhimu kiafya.  Wanawake wengi Tanzania watumia tumbaku

Kuhusu madhara yake kwenye misitu, kilimo cha tumbaku huchangia asilimia tano ya uharibifu wa misitu ulimwenguni kote na pia huchangia pakubwa kuangamia kwa vyanzo muhimu vya maji.

Vyanzo: DPAE, AFPE

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW