1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaNiger

AU yazungumzia hali ya afya ya rais aliyepinduliwa Niger

11 Agosti 2023

Umoja wa Afrika umeelezea wasiwasi wake mkubwa kuhusu taarifa ya hali mbaya ya kiafya inayomkabili Rais wa Niger aliyepinduliwa Mohamed Bazzoum.

Niger US-Außenminister Antony Blinken mit ehem. Präsident Bazoum
Rais aliyepinduliwa nchini Niger Mohammed Bazoum (kulia) alipokutana na Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Marekani, Antony Blinken mjini Niamey, Niger mwezi Machi mwaka 2023Picha: Presidency of Niger/AA/picture alliance

Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Afrika, Moussa Faki Mahamat amesema vitendo vinavyodaiwa kufanywa na viongozi wa mapinduzi dhidi ya Bazzoum havikubaliki.

Mkuu wa shirika la haki za binaadamu la Umoja wa Mataifa, Volker Turk, mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya, Josep Borrell na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres pia wamezungumzia kuhusu hali mbaya aliyonayo Bazoum na familia yake.

Wakati huo huo, wakuu wa kijeshi wa Jumuia ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi, ECOWAS watakutana wiki ijayo kuuzungumzia mzozo wa Niger.

Duru za kijeshi zimeeleza leo kuwa maafisa hao wa kijeshi watakutana Ghana kuandaa mipango ya uwezekano wa kuivamia Niger kijeshi.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW