1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
UgaidiAustralia

Australia kuweka sheria kali zaidi ya umiliki wa silaha

15 Desemba 2025

Viongozi wa Australia wameafikiana Jumatatu kuweka sheria kali zaidi ya umiliki wa silaha baada ya tukio baya zaidi la mauaji lililotokea Jumapili.

Sydney | Raia wa Australia wakiomboleza mauaji hayo yaliyopelekea watu 15 kuuawa
Watu na viongozi wakiomboleza mauaji hayo mjini Sydney-Australia ambapo watu 15 wameuawaPicha: Mark Baker/AP Photo/dpa/picture alliance

Washambuliaji waliwauwa watu 15 kwenye  Ufukwe wa Bondi mjini Sydney wakati wakiadhimisha sikukuu ya Kiyahudi ya Hannukah. Washambuliaji walikuwa baba na mwanawe wa kiume. Baba mwenye umri wa miaka 50 aliuawa kwenye eneo la tukio baada ya kupigwa risasi na polisi, huku mwanawe mwenye umri wa miaka 24 akitiwa nguvuni baada ya kujeruhiwa.

Tukio hilo lililolaaniwa na viongozi mbalimbali duniani lilitajwa kama shambulizi la kigaidi, huku Waziri Mkuu wa Australia, Anthony Albanese, akitangaza kuwa bendera zitapepea nusu mlingoti kuomboleza mauaji hayo.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW