1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Baadhi ya wakaazi wazuiwa kujiandikisha kama wapiga kura DRC

Zuberi Ally3 Februari 2023

Baadhi ya wakaazi wa mji wa Kalemie wamenyimwa haki ya kujiandikisha kama wapiga kura kwa kudaiwa kutokuwa raia halisi wa Kongo

Demokratische Republik Kongo | symbolisches Wahllokal in Beni
Picha: Alexis Huguet/AFP/Getty Images

Wakati tume ya uchaguzi nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo ikiendelea na zoezi la kurekebisha daftari la wapigakura, baadhi ya wakaazi wa mji wa Kalemie wamejikuta wakinyimwa haki ya kujiandikisha kwenye daftari hilo kwa kudaiwa kutokuwa raia halisi wa Kongo.

Lakini pia raia wanawalalamikia watumishi wa tume hiyo ya CENI.

Kila kukicha, raia wanajitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura. Vituo 25 vimetengwa mjini Kalemie kwaajili ya kujiandikisha, miongoni mwa vituo hivyo ni Kichanga, ambako raia wenye asili ya Rwanda wametolewa kwenye foleni na wakaazi wa Kalemie kwa madai kuwa hawastahili kupata kitambulisho hicho.

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo inajiandaa kwa uchaguzi mkuu baadaye mwaka huu.Picha: Dai Kurokawa/dpa/picture alliance

Upande wao mashirika ya kiraia mjini Kalemie kupitia kiongozi wao Byaese Issa wamewaomba raia wenye asili ya kigeni kufuata sheria za nchi Ili kupata uraia wa cchi hii.

Upinzani wakosoa zoezi la usajili wa wapigakura nchini Congo

Wakati hayo yakitokea, raia wa mjini Kalemie wanalalamikia namna maafisa wa tume huru ya uchaguzi CENI wanavyofanya kazi, kwa kuwapa vitambulisho watu ambao hawajafuata utaratibu

Ikumbukwe kuwa utowaji wa vitambulisho hivyo  utadumu kwa muda wa mwezi mmoja

Zuberi Ally DW, kalemie DRC

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW