1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Upinzani wa Kongo wataka wafuasi kupinga matokeo ya uchaguzi

19 Januari 2024

Wagombea watatu wa upinzani wawataka wafuasi wao kuonyesha kukatoridhishwa na matokeo ya uchaguzi katika siku ya uapisho wa Rais Felix Tshisekedi, Januari 20, 2024.

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo | Rais Felix Tshisekedi
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Felix Tshisekedi anatarajiwa kuapishwa Jumamosi Januari 20, 2024 baada ya ushindi katika uchaguzi wa Disemba 20, 2023Picha: AFP

Hata hivyo, Moise Katumbi, Martin Fayulu, na Floribert Anzuluni hawajatoa wito wa kufanyika maandamano. Badala yake wamewasihi wafuasi wao kuelezea kutoridhika kwao, kusimama na kusema hapana kutoka kwenye eneo lolote walipo.

Rais Tshisekedi anatarajiwa kuapishwa Jumamosi, Januari 20, 2024 mjini Kinshasa kwa muhula wa pili.

Fayulu aliwaambia waandishi wa habari kwamba wamesitisha maandamano ya umma kwa sababu hawawezi kuwapeleka watu wakauwawe. Amesema Wakongomani wote wanajua kuwa uchaguzi huo ulikuwa sawa na mchezo wa kuigiza.

Desemba 27 mwaka uliopita, upinzani uliitisha maandamano, lakini yalipigwa marufuku na mamlaka na kuzuiwa na polisi. Tshisekedi alishinda katika uchaguzi huo wa Desemba 20, kwa asilimia 73.27 ya kura.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW