1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BAGHDAD: Al-Qaeda yadai kuhusika na mauaji ya Abu Reesha

15 Septemba 2007

Tawi la mtandao wa kigaidi wa Al-Qaeda nchini Irak limesema kuwa lilifanya shambulizi lililomuuwa kiongozi mashuhuri wa Kisunni,Abdul Sattar Abu Reesha katika Wilaya ya Al-Anbar.Abu Reesha alikuwa akiongoza kundi linaloshirikiana na majeshi ya Marekani kupambana na magaidi wa Al-Qaeda katika wilaya ya Anbar.

Juma lililopita,Rais wa Marekani,George W.Bush alikutana na Abu Reesha,alipofanya ziara yake ya ghafula nchini Irak.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW