1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Baghdad. Polisi wanane wauwawa.

27 Oktoba 2006

Shambulio dhidi ya mlolongo wa magari ya polisi kaskazini mwa mji wa Baghdad limesababisha kuuwawa kwa polisi wanane, ikiwa ni pamoja na kamanda mmoja.

Shambulio hilo lilitokea katika mji wenye ghasia wa Baquba, kilometa 60 kaskazini ya Baghdad.

Mapema jana Alhamis , watu wenye silaha wameshambulia kituo kimoja cha polisi maalum wa Iraq katika mji mwingine karibu na Baquba, na kuuwa polisi sita na kuwajeruhi wengine 10.

Baquba ni ngome kuu ya wapiganaji wa Kisunni wanaopambana na majeshi ya Marekani pamoja na serikali inayoongozwa na Washia.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW