BAGHDAD: Shambulizi la bomu Irak limeua watu 6
16 Oktoba 2007Matangazo
Hadi watu 6 wameuawa mjini Baghdad katika shambulizi la bomu lililotegwa ndani ya gari. Wengine 25 pia wamejeruhiwa katika shambulizi hilo ambalo lililenga wanajeshi waliokuwa wakipiga doria.Wanajeshi 2 wa Kiiraki ni miongoni mwa wale waliouawa.