1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BAGHDAD: Usalama waimarishwa nchini Irak

13 Oktoba 2005

Wanajeshi wa Marekani na Irak wameongeza juhudi zao kulinda usalama katika maeneo yote ya Irak, katika juhudi za kupunguza mashambulio ya wapiganaji yanayolenga kuivuruga kura ya maoni juu ya mswada wa katiba mpya, iliyopangwa kufanyika Jumamosi ijayo.

Siku moja baada ya bunge kukubaliana kuufanyia marekebisho mswada huo baada ya uchaguzi utakaofanyika mwezi Disemba, mji wa Baghdad umekuwa na utulivu huku siku kuu ya kitafa ya siku nne ikinza nchini humo. Msako umetangazwa, mipaka ya Irak itafungwa hapo kesho na hakuna atakayeruhusiwa kusafiri kutoka mkoa mmoja hadi mwingine.

Wanajeshi wameendelea kuwakasa wanamgambo mjini Baghdad na vitongonji vyake na wanajenga kuta kuzunguka vituo vya kupigia kura kama vile shule.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW