1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Baghdad. Wapiganaji 90 wa al-Qaeda wauwawa.

24 Juni 2007

Jeshi la Marekani limesema kuwa wapiganaji 90 wa kundi la al-Qaeda wameuwawa nchini Iraq katika shambulio kubwa lililofanywa katika jimbo la Diyala siku ya Jumanne.

Majeshi ya Marekani na yale ya Iraq yamesema kuwa yamewakamata wapiganaji wawili waandamizi wa al-Qaeda.

Wengi wa viongozi hao wa wapiganaji wanaaminika kuukimbia mji wa Diyala kabla ya kufanyika operesheni hiyo.

Kwingineko nchini Iraq , wanajeshi saba wa jeshi la Marekani wameuwawa katika mashambulio ya mabomu yalilotegwa kando ya barabara ndani na kuzunguka mji mkuu huo wa Iraq, Baghdad.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW