Baghdad.Mabomu yaua watu 14.
9 Oktoba 2007Matangazo
Mabomu mawili yaliyolipuka katika magari katika mji ulioko kaskazini mwa Iraq wa Baiji yameuwa watu 14 na kuwajeruhi wengine 30. Polisi wa Iraq wamesema kuwa bomu la kwanza lililenga katika msikiti na la pili lililengwa katika nyumba ya mkuu wa polisi wa mji huo. Hii inakuja siku moja baada ya watu 21 kuuwawa katika wimbi la mashambulizi ya mabomu nchini Iraq.