BAGHDAD:Mapigano yapamba moto Iraq
20 Juni 2007Matangazo
Polisi ya Iraq imesema takriban watu 78 wameuwawa na wengine wengi kujeruhiwa baada ya bomu la kutegwa ndani ya gari kuripuka karibu na msikiti wa washia mjini Baghdad.
Shambulio hilo limetokea siku mbili tu baada ya kuondolewa kwa amri ya kutotoka nje mjini humo.
Amri hiyo ilitangazwa kufuatia shambulio dhidi ya msikiti wa dhahabu wa washia mjini Sammarra ili kuzuia ghasia za kulipiziana kisasi.
Taarifa nyingine zinasema wanajeshi wa Marekani wamewauwa watu 23 wanaoshukiwa kuwa wanamgambo.
Hii imefuatia opresheni iliyoanzishwa na wanajeshi hao dhidi ya wapiganaji wa kundi la Alqaeda na wanamgambo wakisunni katika mji wa Baquba.