1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BAGHDAD:Moto wazuka kwenye kituo cha jeshi la Marekani nchini Irak

11 Oktoba 2006

Moto uliozuka kwenye kituo cha kijeshi cha Marekani mjini Baghdad ulisababisha miripuko kadhaa mikubwa.

Habari zinasema moto huo ulitokea kwenye bohari ya silaha, lakini hadi sasa hakuna habari iwapo umesababisha madhara yoyote.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na jeshi la Marekani,miripuko hiyo ilisababishwa na joto kali.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW