BAGHDAD:Waziri Mkuu Nuri Maliki ajitetea
15 Julai 2007Matangazo
Waziri Mkuu wa Irak bwana Nuri al Maliki amepinga lawama zinazotolewa dhidi ya serikali yake na amejitetea kwa kusema kuwa mazingira ya kivita ndiyo yanayochelewesha utekelezaji wa malengo yanayokusudiwa na serikali yake.
Bwana Maliki ameeleza kuwa ujiingizaji kutoka nje pia unachangia katika mazingira hayo.Waziri mkuu huyo pia ameitaka Mrekani impe muda zaidi ili aweze kufikia malengo yanayokusudiwa.
Hilo ni tamko la kwanza la waziri mkuu Maliki tokea Marekani itoe ripoti yake juu ya hali ya sasa nchini Irak.