1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ban Ki-Moon ahimiza suluhisho la Darfur

P.Martin5 Septemba 2007

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon amekwenda Juba,mji wa kusini mwa Sudan.

Lengo la ziara ya Katibu Mkuu Ban,ni kujaribu kuhimiza utekelezaji wa makubaliano ya amani ya yaliyotiwa saini mwaka 2005.

Hapo awali Ban alikutana na Rais Omar el-Bashir wa Sudan mjini Khartoum na alisema, walijadiliana njia za kuharakisha kupeleka Darfur vikosi vya Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika.

Vile vile alimuarifu Rais el-Bashir juu ya juhudi zake na mwenyekiti wa Umoja wa Afrika,kuhimiza majadiliano ya amani kuhusu Darfur pamoja na makubaliano kamili ya amani.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW