Migogoro
Baraza Kuu UN lataka amani, vita visitishwe haraka Ukraine
25 Februari 2026
Matangazo
Azimio la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa linalotaka pia amani ya kudumu ya Ukraine na kuheshimu sheria za kimataifa, limepitishwa Jumanne ikiwa ni miaka minne tangu Moscow ilipoivamia Ukraine.
Marekani yasita kupiga kura kuliunga mkono azimio
Mataifa 107 wanachama wa Umoja wa Mataifa yalipigia kura ya kuunga mkono azimio hilo wakati 12 yamepinga. Nchi 51 hazikupiga kura ya kulikataa au kuliunga mkono ikiwemo Marekani.
Rais wa Baraza Kuu la umoja huo Annalena Baerbock ameizungumzia hatua hiyo na kusisitiza kuwa amani itapatikana na kuwa ya kudumu kama itazingatia kanuni za Mkataba wa Umoja wa Mataifa na kuheshimu uhuru wa Ukraine.