1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Baraza la Usalama kuiondolea Somalia vikwazo vya silaha

1 Desemba 2023

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo litapiga kura ya kuondoa vikwazo vya mwisho vya silaha kwa serikali ya Somalia na vikosi vyake vya ulinzi.

Machafuko Somalia
Somalia iliwekewa vikwazo vya silaha na Umoja wa Mataifa.Picha: Hassan Ali ElmiAFP/ Getty Images

Haya yamesemwa na wanadiplomasia, zaidi ya miaka 30 baada ya nchi hiyo kuwekewa vikwazo vya kununua silaha. Baraza hilo la usalama lenye wanachama 15 katika kura hiyo linatarajiwa kukubali rasimu mbili za maazimio zilizoandikwa na Uingereza.

Mojawapo ya rasimu hizo ni ya kuondoa kikamilifu vikwazo vya silaha ilivyowekewa Somalia na nyengine ni ya kuliwekea vikwazo vya silaha kundi la kigaidi la Al Shabaab lililo na mafungamano na mtandao wa Al Qaeda.

Soma pia: Somalia karibu Kwenye jumuiya ya Afrika Mashariki

Baraza hilo la usalama liliiwekea serikali ya Somalia vikwazo mwaka 1992 ili kukata usambazaji wa silaha kwa wababe wa kivita waliokuwa wamempindua dikteta Mohamed Siad Barre na kuitumbukiza nchi hiyo ya Pembe ya Afrika katika vita vya wenyewe kwa wenyewe.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW