1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaIran

UN kupiga kura kuhusu kurejesha vikwazo dhidi ya Iran

19 Septemba 2025

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linatarajiwa Ijumaa kupiga kura ya kurejesha vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Iran kutokana na hatua ya kufufua mpango wake wa nyuklia.

Uingereza, Ufaransa na Ujerumani ambazo zilitia saini mpango wa mwaka 2015 ulionuia kuizuia  Tehran kumiliki silaha za nyuklia , wanadai kuwa Iran imevunja ahadi zake chini ya mkataba huo. China na Urusi zinapinga hatua ya kurejeshwa kwa vikwazo hivyo.

Lakini vyanzo vya kidiplomasia vinatarajia kuwa azimio hilo halitapata kura tisa zinazohitajika ili kudumisha hali ya sasa na kwamba vikwazo hivyo vinatarajiwa kuanzishwa tena. Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema vikwazo hivyo vinatarajiwa kurejeshwa mwishoni mwa mwezi huu.

 

Tanbihi ya Mhariri: Makala hii awali ilijumuisha picha kutoka shirika la SalamPix. Iliondolewa tarehe 12 Machi 2026 baada ya Picture Alliance na Imago kutuarifu kuwa walikuwa wanaondoa picha za SalamPix kutokana na wasiwasi kuhusu chanzo chake na uwezekano wa kuwa zimehaririwa.          

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW