1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Baraza la Usalama la UN lagawanyika kuhusu Gaza

15 Novemba 2025

Marekani na Urusi zimewasilisha rasimu pinzani za maazimio kuhusu mzozo wa Gaza kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, na kuibua hali ya mvutano kati ya mataifa hayo mawili yenye kura ya turufu katika baraza hilo.

Makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York, Marekani
Mkutano wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa mnamo Mei 20, 2022Picha: Manuel Elias/UN Photo/Xinhua/picture alliance

Wajumbe wamesema kura hiyo inaweza kufanyika mapema wiki ijayo. Rasimu ya Marekani inalenga kuwezesha utekelezaji wa mpango wa amani wa Rais Donald Trump kwa eneo zima la Mashariki ya Kati.

Kwa upande wake, Urusi  imewasilisha azimio lake, ambalo linajumuisha kuitambua Palestina kama taifa, huku China ikiashiria kuwa tayari kuiunga mkono rasimu ya Urusi.

Misri, Qatar, Umoja wa Falme za Kiarabu, Pakistan, Saudi Arabia, Jordan na Uturuki zimeunga mkono hadharani rasimu ya Marekani.

Urusi, China na Marekani zote zinashikilia kura ya turufu katika baraza hilo, hii ikimaanisha kuwa azimio lolote wanalolipinga haliwezi kupitishwa.