1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Barca na City washinda mechi za awali za Champions

26 Oktoba 2023

Manchester City ikiongozwa na Erling Haaland ilishinda mabao 3-1 dhidi ya Young Boys na kuongoza kundi G, ikifuatiwa na RB Leipzig iliyopata ushindi dhidi ya Red Star Belgrade.

RB Leipzig - Manchester City / Champions League
Picha: Odd Andersen/AFP

Mabingwa watetezi wa michuano ya ligi ya mabingwa Ulaya, Manchester City wameanza vyema mbio za ubingwa sambamba na Barcelona na kuinyemelea hatua ya makundi.

Manchester City ikiongozwa na Erling Haaland ilishinda mabao 3-1 dhidi ya Young Boys na kuongoza kundi G, ikifuatiwa na RB Leipzig iliyopata ushindi dhidi ya Red Star Belgrade.

Barcelona, iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Shakhtar Donesk katika kundi H, huku Porto ikiifunga Royal Antwerp mabao 4-1.

Ushindi huu unawaongezea matumaini kwenye mechi za mwisho wa wiki, wakati Barcelona itakapokwaana na Real Madrid katika La Liga Classico na Man City dhidi ya Manchester United katika Derby ya PL.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW