1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Barcelona kumkosa Yamal dhidi ya Newcastle

17 Septemba 2025

Mabingwa wa Uhispania Barcelona watamkosa nyota wao Lamine Yamal katika mechi yao ya ufunguzi Alhamis watakapochuana na Newcastle United ya England.

Winga wa Barcelona Lamine Yamal akisherehekea kufunga goli
Winga wa Barcelona Lamine Yamal akisherehekea kufunga goliPicha: Altaf Qadri/AP/dpa/picture alliance

Barcelona imesema kuwa Yamal hayumo katika kikosi kinachoelekea England kupambana na Newcastle katika mechi hiyo ya kwanza ya makundi.

Yamal tayari alikuwa ameikosa mechi ya La Liga ya Barcelona mwishoni mwa wiki walipopambana na Valencia na kushinda 6-0, kufuatia jeraha alilopata katika eneo la sehemu nyeti.

Kocha wa Barca Hansi Flick amesema alighadhabishwa na hatua ya timu ya taifa ya Uhispania kumchezesha Yamal katika mechi zao za kuwania kufuzu Kombe la Dunia ambazo walizishinda kwa urahisi.

Nyota huyo alipata jeraha hilo wakati wa mechi hizo za kimataifa.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW