1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BARCELONA: Washukiwa ugaidi wamekamatwa Hispania

27 Juni 2007

Wanaume 3 wanaotuhumiwa kuajiri watu watakaoweza kutumiwa kama magaidi kwa niaba ya mtandao wa al-Qaeda,wamekamatwa nchini Hispania.Polisi imesema, wanaume hao watatu walikamatwa mjini Barcelona na wanahusika na kundi linaloitwa,“Shirikisho la al-Qaeda katika eneo la Kiislamu la Maghreb“.Hivi karibuni,maafisa wa Ulaya wanaopambana na ugaidi, walionya kwamba chama kilichokuwa na makao yake nchini Algeria,kinajaribu kueneza harakati zake barani Ulaya.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW