Bayern, Chelsea na kibarua cha barani Ulaya
9 Machi 2015![UEFA Champions League Arjen Robben David Alaba Schachtar Donezk FC Bayern München Ukraine](https://static.dw.com/image/18265435_800.webp)
Matangazo
Chelsea, iliyoshinda Kombe la 2012, ilipata goli la ugenini katika sare ya 1-1 na Paris St Germain wakati mabinhwa wa 2013 Bayern Munich wakitoka sare ya bila na Shakhtar Donetsk mjini Lviv.
Kesho Jumanne, Porto itakutana na Basel baada ya sare ya 1-1 nchini Uswisi wakati Real Madrid wakitaraji kuwa faida yao ya mabao mawili kwa sifuri itatosha kuwapa tikiti ya robo fainali nyumbani kwa Schalke.
Mwandishi: Bruce Amani/AFP/reuters
Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman