1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BEIJING: Wachimba migodi 102 wamo hatarini

8 Agosti 2005

Wachimba migodi 102 wamekwama katika mgodi wa makaa ya mawe uliofurika, kusini mwa China. Ajali hiyo imetokea katika mkoa wa Guangdong yapata mita 420 chini ya ardhi na waokoaji wanajaribu kuyavuta maji kutumia mitambo ili kuwaokoa wachimba migodi hao.

Migodi nchini China ndio migodi hatari kabisa duniani, huku wachimba migodi 2,700 wakiuwawa katika migodi hiyo kila miezi sita ya mwanzo kila mwaka.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW