1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BEIRUT: Jeshi laendelea na operesheni ya kuwangóa wanamgambo

23 Juni 2007

Jeshi la Lebanon limesema,linaendelea na operesheni za kijeshi katika kambi ya wakimbizi wa Kipalestina ya Nahr al-Bared,kaskazini mwa Lebanon.Lengo la operesheni hiyo ni kuwangóa wapiganaji wa kundi la Fatah al-Islam waliobakia katika kambi hiyo.Hapo awali,waziri wa ulinzi wa Lebanon alisema,wanamgambo hao wa Kiislamu waliojificha kambini wameshindwa,na sasa jeshi linashughulika na operesheni ya kuisafisha kambi hiyo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW