BEIRUT:Uchunguzi juu ya kifo cha Hariri utaendelea
1 Septemba 2005Matangazo
Uchunguzi juu ya kuuliwa kwa waziri mkuu wa zamani wa Lebabon Rafik Hariri utaendelea.
Kwa mujibu wa Kiongozi wa kikundi cha uchunguzi huo ambaye ni mwendesha mashtaka wa kijerumani Detlev Mehlis ni kwamba ni watu wengi walioshiriki kwenye mauaji hayo yaliyofanyika februari kuliko wale watano waliokamatwa na kushukiwa hadi sasa.
Amesema ili kupata ukweli msaada wa Syria ni muhimu licha ya uchunguzi huo kuonyesha kwamba hadi sasa hakuna afisa yoyote wa kisyria aliyehusika na mauaji hayo.