1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Berlin. Aliyejaribu kumuua Hitler akumbukwa.

16 Novemba 2007

Katika sherehe maalum mjini Berlin, waziri wa ulinzi wa Ujerumani Franz Josef Jung ameadhimisha miaka 100 ya kuzaliwa kwa Claus Schenk von Stauffenberg, afisa wa jeshi la Ujerumani , ambaye alijaribu kumuua kiongozi wa wanazi Adolf Hittler wakati wa vita vikuu vya pili vya dunia. Jung amekitaja kitendo cha jaribio la kumuua Hitler , tukio la ukombozi, na kusema kuwa von Stauffenberg alikuwa mfano kwa majeshi ya Ujerumani. Mwanahistoria wa Ujerumani , hata hivyo, ameonya dhidi ya kumfanya von Stauffenberg kuwa shujaa wakati alikuwa akiunga mkono malengo ya utawala wa Wanazi kwa miaka kadha kabla ya kugeuka.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW